عَسَىٰ رَبُّهُۥٓ إِن طَلَّقَكُنَّ أَن يُبۡدِلَهُۥٓ أَزۡوَٰجًا خَيۡرٗا مِّنكُنَّ مُسۡلِمَٰتٖ مُّؤۡمِنَٰتٖ قَٰنِتَٰتٖ تَـٰٓئِبَٰتٍ عَٰبِدَٰتٖ سَـٰٓئِحَٰتٖ ثَيِّبَٰتٖ وَأَبۡكَارٗا
Asaa Mola wake Mlezi, akikupeni talaka, akampa wake wengine badala yenu nyinyi, walio bora kuliko nyinyi, wanynyekevu, Waumini, wat'awa, walio tubu, wenye kushika ibada, wafanyao kheri, wajane na wanawari.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Linalotarajiwa kwa Mola wake iwapo atawaacha nyinyi, enyi wake zake, ni amuoze yeye, badala yenu nyinyi, wake wanyenyekevu kwa Mwenyezi Mungu kwa kumtii, wenye kumuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, wenye kumtii Mwenyezi mungu, wenye kurudi kwenye yale anayoyapenda Mwenyezi Mungu ya kumtii Yeye, wenye kumuabudu kwa wingi, wenye kufunga sana, wakiwa wake wakuu miongoni mwao na wanawali.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس