وَحُورٌ عِينٞ

Na Mahurulaini,


كَأَمۡثَٰلِ ٱللُّؤۡلُوِٕ ٱلۡمَكۡنُونِ

Walio kama mfano wa lulu zilio hifadhiwa.


جَزَآءَۢ بِمَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ

Ni malipo kwa waliyo kuwa wakiyatenda.


لَا يَسۡمَعُونَ فِيهَا لَغۡوٗا وَلَا تَأۡثِيمًا

Humo hawatasikia porojo wala maneno ya dhambi,


إِلَّا قِيلٗا سَلَٰمٗا سَلَٰمٗا

Isipo kuwa maneno ya Salama, Salama.


وَأَصۡحَٰبُ ٱلۡيَمِينِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡيَمِينِ

Na wale wa mkono wa kulia, ni yepi yatakuwa ya wa kuliani?


فِي سِدۡرٖ مَّخۡضُودٖ

Katika mikunazi isiyo na miba,


وَطَلۡحٖ مَّنضُودٖ

Na migomba iliyo pangiliwa,


وَظِلّٖ مَّمۡدُودٖ

Na kivuli kilicho tanda,


وَمَآءٖ مَّسۡكُوبٖ

Na maji yanayo miminika,


وَفَٰكِهَةٖ كَثِيرَةٖ

Na matunda mengi,



الصفحة التالية
Icon