لَّا مَقۡطُوعَةٖ وَلَا مَمۡنُوعَةٖ

Hayatindikii wala hayakatazwi,


وَفُرُشٖ مَّرۡفُوعَةٍ

Na matandiko yaliyo nyanyuliwa.


إِنَّآ أَنشَأۡنَٰهُنَّ إِنشَآءٗ

Hakika Sisi tutawaumba (Mahurulaini) upya,


فَجَعَلۡنَٰهُنَّ أَبۡكَارًا

Na tutawafanya vijana,


عُرُبًا أَتۡرَابٗا

Wanapendana na waume zao, hirimu moja.


لِّأَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ

Kwa ajili ya watu wa kuliani.


ثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأَوَّلِينَ

Fungu kubwa katika wa mwanzo,


وَثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأٓخِرِينَ

Na fungu kubwa katika wa mwisho.


وَأَصۡحَٰبُ ٱلشِّمَالِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلشِّمَالِ

Na watu wa kushotoni; je ni yepi ya wa kushotoni?


فِي سَمُومٖ وَحَمِيمٖ

Katika upepo wa moto, na maji yanayo chemka,


وَظِلّٖ مِّن يَحۡمُومٖ

Na kivuli cha moshi mweusi,



الصفحة التالية
Icon