لَّا بَارِدٖ وَلَا كَرِيمٍ

Si cha kuburudisha wala kustarehesha.


إِنَّهُمۡ كَانُواْ قَبۡلَ ذَٰلِكَ مُتۡرَفِينَ

Hakika hao walikuwa kabla ya haya wakiishi maisha ya anasa.


وَكَانُواْ يُصِرُّونَ عَلَى ٱلۡحِنثِ ٱلۡعَظِيمِ

Na walikuwa wakishikilia kufanya madhambi makubwa,


وَكَانُواْ يَقُولُونَ أَئِذَا مِتۡنَا وَكُنَّا تُرَابٗا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَبۡعُوثُونَ

Na walikuwa wakisema: Tutakapo kufa na tukawa udongo na mafupa, ati ndio tutafufuliwa?


أَوَءَابَآؤُنَا ٱلۡأَوَّلُونَ

Au baba zetu wa zamani?


قُلۡ إِنَّ ٱلۡأَوَّلِينَ وَٱلۡأٓخِرِينَ

Sema: Hakika wa zamani na wa mwisho


لَمَجۡمُوعُونَ إِلَىٰ مِيقَٰتِ يَوۡمٖ مَّعۡلُومٖ

Bila ya shaka watakusanywa kwa wakati wa siku maalumu.


ثُمَّ إِنَّكُمۡ أَيُّهَا ٱلضَّآلُّونَ ٱلۡمُكَذِّبُونَ

Kisha nyinyi, mlio potea, mnao kanusha,


لَأٓكِلُونَ مِن شَجَرٖ مِّن زَقُّومٖ

Kwa yakini mtakula mti wa Zaqqumu.



الصفحة التالية
Icon