ءَأَنتُمۡ أَنشَأۡتُمۡ شَجَرَتَهَآ أَمۡ نَحۡنُ ٱلۡمُنشِـُٔونَ

Ni nyinyi mlio uumba mti wake au Sisi ndio Waumbaji?


نَحۡنُ جَعَلۡنَٰهَا تَذۡكِرَةٗ وَمَتَٰعٗا لِّلۡمُقۡوِينَ

Sisi tumeufanya uwe ni ukumbusho na manufaa kwa walioko nyikani.


فَسَبِّحۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلۡعَظِيمِ

Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkuu.


۞فَلَآ أُقۡسِمُ بِمَوَٰقِعِ ٱلنُّجُومِ

Basi naapa kwa maanguko ya nyota,


وَإِنَّهُۥ لَقَسَمٞ لَّوۡ تَعۡلَمُونَ عَظِيمٌ

Na hakika bila ya shaka hichi ni kiapo kikubwa, laiti mngeli jua!


إِنَّهُۥ لَقُرۡءَانٞ كَرِيمٞ

Hakika hii bila ya shaka ni Qur'ani Tukufu,


فِي كِتَٰبٖ مَّكۡنُونٖ

Katika Kitabu kilicho hifadhiwa.


لَّا يَمَسُّهُۥٓ إِلَّا ٱلۡمُطَهَّرُونَ

Hapana akigusaye ila walio takaswa.


تَنزِيلٞ مِّن رَّبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Ni uteremsho unao toka kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.


أَفَبِهَٰذَا ٱلۡحَدِيثِ أَنتُم مُّدۡهِنُونَ

Ni maneno haya ndiyo nyinyi mnayapuuza?



الصفحة التالية
Icon