وَتَجۡعَلُونَ رِزۡقَكُمۡ أَنَّكُمۡ تُكَذِّبُونَ

Na badala ya kushukuru kwa riziki yenu mnafanya kuwa mnakadhibisha?


فَلَوۡلَآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلۡحُلۡقُومَ

Yawaje basi itakapo fika roho kwenye koo,


وَأَنتُمۡ حِينَئِذٖ تَنظُرُونَ

Na nyinyi wakati huo mnatazama!


وَنَحۡنُ أَقۡرَبُ إِلَيۡهِ مِنكُمۡ وَلَٰكِن لَّا تُبۡصِرُونَ

Na Sisi tuko karibu zaidi naye kuliko nyinyi.


فَلَوۡلَآ إِن كُنتُمۡ غَيۡرَ مَدِينِينَ

Na lau kuwa nyinyi hamumo katika mamlaka yangu,


تَرۡجِعُونَهَآ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ

Kwanini hamuirudishi hiyo roho, ikiwa nyinyi mnasema kweli?


فَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلۡمُقَرَّبِينَ

Basi akiwa miongoni mwa walio karibishwa,


فَرَوۡحٞ وَرَيۡحَانٞ وَجَنَّتُ نَعِيمٖ

Basi ni raha, na manukato, na Bustani zenye neema.


وَأَمَّآ إِن كَانَ مِنۡ أَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ

Na akiwa katika watu wa upande wa kulia,


فَسَلَٰمٞ لَّكَ مِنۡ أَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ

Basi ni Salamu kwako uliye miongoni mwa watu wa upande wa kulia.



الصفحة التالية
Icon