وَلَا تُطِعۡ كُلَّ حَلَّافٖ مَّهِينٍ

Wala usimt'ii kila mwingi wa kuapa wa kudharauliwa,


هَمَّازٖ مَّشَّآءِۭ بِنَمِيمٖ

Mtapitapi, apitaye akifitini,


مَّنَّاعٖ لِّلۡخَيۡرِ مُعۡتَدٍ أَثِيمٍ

Mwenye kuzuia kheri, dhaalimu, mwingi wa madhambi,


عُتُلِّۭ بَعۡدَ ذَٰلِكَ زَنِيمٍ

Mkavu, na juu ya hayo, mshari, amejipachika tu.


أَن كَانَ ذَا مَالٖ وَبَنِينَ

Ati kwa kuwa ana mali na watoto!


إِذَا تُتۡلَىٰ عَلَيۡهِ ءَايَٰتُنَا قَالَ أَسَٰطِيرُ ٱلۡأَوَّلِينَ

Anapo somewa Aya zetu, husema: Hizi ni simulizi za uwongo za watu wa zamani!


سَنَسِمُهُۥ عَلَى ٱلۡخُرۡطُومِ

Tutamtia kovu juu ya pua yake.


إِنَّا بَلَوۡنَٰهُمۡ كَمَا بَلَوۡنَآ أَصۡحَٰبَ ٱلۡجَنَّةِ إِذۡ أَقۡسَمُواْ لَيَصۡرِمُنَّهَا مُصۡبِحِينَ

Hakika tumewajaribu hawa kama tulivyo wajaribu wale wenye shamba, walipo apa kwamba watayavuna mazao yake itakapo kuwa asubuhi.


وَلَا يَسۡتَثۡنُونَ

Wala hawakusema: Mungu akipenda!



الصفحة التالية
Icon