وَلَمۡ أَدۡرِ مَا حِسَابِيَهۡ

Wala nisingeli jua nini hisabu yangu.


يَٰلَيۡتَهَا كَانَتِ ٱلۡقَاضِيَةَ

Laiti mauti ndiyo yangeli kuwa ya kunimaliza kabisa.


مَآ أَغۡنَىٰ عَنِّي مَالِيَهۡۜ

Mali yangu hayakunifaa kitu.


هَلَكَ عَنِّي سُلۡطَٰنِيَهۡ

Madaraka yangu yamenipotea.


خُذُوهُ فَغُلُّوهُ

(Pasemwe): Mshikeni! Mtieni pingu!


ثُمَّ ٱلۡجَحِيمَ صَلُّوهُ

Kisha mtupeni Motoni!


ثُمَّ فِي سِلۡسِلَةٖ ذَرۡعُهَا سَبۡعُونَ ذِرَاعٗا فَٱسۡلُكُوهُ

Tena mtatizeni katika mnyororo wenye urefu wa dhiraa sabiini!


إِنَّهُۥ كَانَ لَا يُؤۡمِنُ بِٱللَّهِ ٱلۡعَظِيمِ

Kwani huyo hakika alikuwa hamuamini Mwenyezi Mungu Mtukufu,


وَلَا يَحُضُّ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلۡمِسۡكِينِ

Wala hahimizi kulisha masikini.


فَلَيۡسَ لَهُ ٱلۡيَوۡمَ هَٰهُنَا حَمِيمٞ

Basi leo hapa hana jamaa wa kumwonea uchungu,



الصفحة التالية
Icon