يُبَصَّرُونَهُمۡۚ يَوَدُّ ٱلۡمُجۡرِمُ لَوۡ يَفۡتَدِي مِنۡ عَذَابِ يَوۡمِئِذِۭ بِبَنِيهِ

Ijapo kuwa wataonyeshwa waonane. Atatamani mkosefu lau ajikomboe na adhabu ya siku hiyo kwa kuwatoa fidia wanawe,


وَصَٰحِبَتِهِۦ وَأَخِيهِ

Na mkewe, na nduguye,


وَفَصِيلَتِهِ ٱلَّتِي تُـٔۡوِيهِ

Na jamaa zake walio kuwa wakimkimu,


وَمَن فِي ٱلۡأَرۡضِ جَمِيعٗا ثُمَّ يُنجِيهِ

Na wote waliomo duniani, kisha aokoke yeye.


كَلَّآۖ إِنَّهَا لَظَىٰ

La, hasha! Kwa hakika huo ni Moto mkali kabisa,


نَزَّاعَةٗ لِّلشَّوَىٰ

Unao babua ngozi ya kichwa!


تَدۡعُواْ مَنۡ أَدۡبَرَ وَتَوَلَّىٰ

Utamwita kila aliye geuza mgongo na akageuka.


وَجَمَعَ فَأَوۡعَىٰٓ

Na akakusanya mali, kisha akayahifadhi.


۞إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ خُلِقَ هَلُوعًا

Hakika mtu ameumbwa na papara.


إِذَا مَسَّهُ ٱلشَّرُّ جَزُوعٗا

Inapo mgusa shari hupapatika.



الصفحة التالية
Icon