كَلَّا لَا وَزَرَ

La! Hapana pa kukimbilia!


إِلَىٰ رَبِّكَ يَوۡمَئِذٍ ٱلۡمُسۡتَقَرُّ

Siku hiyo pa kutua ni kwa Mola wako Mlezi tu.


يُنَبَّؤُاْ ٱلۡإِنسَٰنُ يَوۡمَئِذِۭ بِمَا قَدَّمَ وَأَخَّرَ

Siku hiyo ataambiwa aliyo yatanguliza na aliyo yaakhirisha.


بَلِ ٱلۡإِنسَٰنُ عَلَىٰ نَفۡسِهِۦ بَصِيرَةٞ

Bali mtu ni hoja juu ya nafsi yake.


وَلَوۡ أَلۡقَىٰ مَعَاذِيرَهُۥ

Na ingawa atatoa chungu ya udhuru.


لَا تُحَرِّكۡ بِهِۦ لِسَانَكَ لِتَعۡجَلَ بِهِۦٓ

Usiutikisie huu wahyi ulimi wako kwa kuufanyia haraka.


إِنَّ عَلَيۡنَا جَمۡعَهُۥ وَقُرۡءَانَهُۥ

Hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha.


فَإِذَا قَرَأۡنَٰهُ فَٱتَّبِعۡ قُرۡءَانَهُۥ

Tunapo usoma, basi nawe fuatiliza kusoma kwake.


ثُمَّ إِنَّ عَلَيۡنَا بَيَانَهُۥ

Kisha ni juu yetu kuubainisha.


كَلَّا بَلۡ تُحِبُّونَ ٱلۡعَاجِلَةَ

Hasha! Bali nyinyi mnapenda maisha ya duniani,



الصفحة التالية
Icon