وَتَذَرُونَ ٱلۡأٓخِرَةَ

Na mnaacha maisha ya Akhera.


وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ نَّاضِرَةٌ

Zipo nyuso siku hiyo zitao ng'ara,


إِلَىٰ رَبِّهَا نَاظِرَةٞ

Zinamwangallia Mola wao Mlezi.


وَوُجُوهٞ يَوۡمَئِذِۭ بَاسِرَةٞ

Na zipo nyuso siku hiyo zitakao kunjana.


تَظُنُّ أَن يُفۡعَلَ بِهَا فَاقِرَةٞ

Zitajua ya kuwa zitafikiwa na livunjalo uti wa mgongo.


كَلَّآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلتَّرَاقِيَ

La, hasha! (Roho) itakapo fikia kwenye mafupa ya koo,


وَقِيلَ مَنۡۜ رَاقٖ

Na pakasemwa: Nani wa kumganga?


وَظَنَّ أَنَّهُ ٱلۡفِرَاقُ

Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa huko ndiko kufariki;


وَٱلۡتَفَّتِ ٱلسَّاقُ بِٱلسَّاقِ

Na utapo ambatishwa muundi kwa muundi,


إِلَىٰ رَبِّكَ يَوۡمَئِذٍ ٱلۡمَسَاقُ

Siku hiyo ndiyo kuchungwa kupelekwa kwa Mola wako Mlezi!


فَلَا صَدَّقَ وَلَا صَلَّىٰ

Kwa sababu hakusadiki, wala hakusali.



الصفحة التالية
Icon