لِأَيِّ يَوۡمٍ أُجِّلَتۡ

Kwa siku gani hiyo wamewekewa muda huo?


لِيَوۡمِ ٱلۡفَصۡلِ

Kwa siku ya kupambanua!


وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلۡفَصۡلِ

Na nini kitakacho kujuulisha siku ya kupambanua ni nini?


وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao, siku hiyo hao wanao kanusha!


أَلَمۡ نُهۡلِكِ ٱلۡأَوَّلِينَ

Kwani hatukuwaangamiza walio tangulia?


ثُمَّ نُتۡبِعُهُمُ ٱلۡأٓخِرِينَ

Kisha tukawafuatilizia walio fuatia?


كَذَٰلِكَ نَفۡعَلُ بِٱلۡمُجۡرِمِينَ

Ndio kama hivi tuwatendavyo wakosefu!


وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!


أَلَمۡ نَخۡلُقكُّم مِّن مَّآءٖ مَّهِينٖ

Kwani hatukukuumbeni kwa maji ya kudharauliwa?


فَجَعَلۡنَٰهُ فِي قَرَارٖ مَّكِينٍ

Kisha tukayaweka mahali pa utulivu madhubuti?


إِلَىٰ قَدَرٖ مَّعۡلُومٖ

Mpaka muda maalumu?



الصفحة التالية
Icon