فَقَدَرۡنَا فَنِعۡمَ ٱلۡقَٰدِرُونَ

Tukakadiria na Sisi ni wabora wa kukadiria.


وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!


أَلَمۡ نَجۡعَلِ ٱلۡأَرۡضَ كِفَاتًا

Kwani hatukuifanya ardhi yenye kukusanya


أَحۡيَآءٗ وَأَمۡوَٰتٗا

Walio hai na maiti?


وَجَعَلۡنَا فِيهَا رَوَٰسِيَ شَٰمِخَٰتٖ وَأَسۡقَيۡنَٰكُم مَّآءٗ فُرَاتٗا

Na ndani yake tukaweka milima mirefu yenye kuthibiti, na tunakunywesheni maji matamu?


وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!


ٱنطَلِقُوٓاْ إِلَىٰ مَا كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ

Nendeni kwenye adhabu mliyo kuwa mkiikanusha!


ٱنطَلِقُوٓاْ إِلَىٰ ظِلّٖ ذِي ثَلَٰثِ شُعَبٖ

Nendeni kwenye kivuli chenye mapande matatu!


لَّا ظَلِيلٖ وَلَا يُغۡنِي مِنَ ٱللَّهَبِ

Hakikingi moto, wala hakiwaepushi na mwako.


إِنَّهَا تَرۡمِي بِشَرَرٖ كَٱلۡقَصۡرِ

Hakika Moto huo unatoa macheche kama majumba!



الصفحة التالية
Icon