وَبَنَيۡنَا فَوۡقَكُمۡ سَبۡعٗا شِدَادٗا

Na tukajenga juu yenu saba zenye nguvu?


وَجَعَلۡنَا سِرَاجٗا وَهَّاجٗا

Na tukaifanya taa yenye mwanga na joto;


وَأَنزَلۡنَا مِنَ ٱلۡمُعۡصِرَٰتِ مَآءٗ ثَجَّاجٗا

Na tukateremsha maji yanayo anguka kwa kasi kutoka mawinguni,


لِّنُخۡرِجَ بِهِۦ حَبّٗا وَنَبَاتٗا

Ili tutoe kwayo nafaka na mimea,


وَجَنَّـٰتٍ أَلۡفَافًا

Na mabustani yenye miti iliyo kamatana.


إِنَّ يَوۡمَ ٱلۡفَصۡلِ كَانَ مِيقَٰتٗا

Hakika siku ya uamuzi imewekewa wakati wake,


يَوۡمَ يُنفَخُ فِي ٱلصُّورِ فَتَأۡتُونَ أَفۡوَاجٗا

Siku litapo pulizwa barugumu, nanyi mtakuja kwa makundi,


وَفُتِحَتِ ٱلسَّمَآءُ فَكَانَتۡ أَبۡوَٰبٗا

Na mbingu zitafunguliwa, ziwe milango,


وَسُيِّرَتِ ٱلۡجِبَالُ فَكَانَتۡ سَرَابًا

Na milima itaondolewa na itakuwa kama sarabi.


إِنَّ جَهَنَّمَ كَانَتۡ مِرۡصَادٗا

Hakika Jahannamu inangojea!



الصفحة التالية
Icon