قَالُواْ تِلۡكَ إِذٗا كَرَّةٌ خَاسِرَةٞ

Wanasema: Basi marejeo hayo ni yenye khasara!


فَإِنَّمَا هِيَ زَجۡرَةٞ وَٰحِدَةٞ

Kwa hakika hayo ni ukelele mmoja tu,


فَإِذَا هُم بِٱلسَّاهِرَةِ

Mara watakuwa kwenye uwanda wa mkutano!


هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ مُوسَىٰٓ

Je! Imekufikia hadithi ya Musa?


إِذۡ نَادَىٰهُ رَبُّهُۥ بِٱلۡوَادِ ٱلۡمُقَدَّسِ طُوًى

Mola wake Mlezi alipo mwita katika bonde takatifu la T'uwaa, akamwambia:


ٱذۡهَبۡ إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ إِنَّهُۥ طَغَىٰ

Nenda kwa Firauni. Hakika yeye amezidi jeuri.


فَقُلۡ هَل لَّكَ إِلَىٰٓ أَن تَزَكَّىٰ

Umwambie: Je! Unapenda kujitakasa?


وَأَهۡدِيَكَ إِلَىٰ رَبِّكَ فَتَخۡشَىٰ

Nami nitakuongoa ufike kwa Mola wako Mlezi, upate kumcha.


فَأَرَىٰهُ ٱلۡأٓيَةَ ٱلۡكُبۡرَىٰ

Basi alimwonyesha Ishara kubwa.


فَكَذَّبَ وَعَصَىٰ

Lakini aliikadhibisha na akaasi.



الصفحة التالية
Icon