ثُمَّ أَدۡبَرَ يَسۡعَىٰ

Kisha alirudi nyuma, akaingia kufanya juhudi.


فَحَشَرَ فَنَادَىٰ

Akakusanya watu akanadi.


فَقَالَ أَنَا۠ رَبُّكُمُ ٱلۡأَعۡلَىٰ

Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi mkuu kabisa.


فَأَخَذَهُ ٱللَّهُ نَكَالَ ٱلۡأٓخِرَةِ وَٱلۡأُولَىٰٓ

Basi hapo Mwenyezi Mungu akamshika kumuadhibu kwa la mwisho na la mwanzo.


إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَعِبۡرَةٗ لِّمَن يَخۡشَىٰٓ

Kwa hakika katika haya yapo mazingatio kwa wanao ogopa.


ءَأَنتُمۡ أَشَدُّ خَلۡقًا أَمِ ٱلسَّمَآءُۚ بَنَىٰهَا

Je! Ni vigumu zaidi kukuumbeni nyinyi au mbingu? Yeye ndiye aliye ijenga!


رَفَعَ سَمۡكَهَا فَسَوَّىٰهَا

Akainua kimo chake, na akaitengeneza vizuri.


وَأَغۡطَشَ لَيۡلَهَا وَأَخۡرَجَ ضُحَىٰهَا

Na akautia giza usiku wake, na akautokeza mchana wake.


وَٱلۡأَرۡضَ بَعۡدَ ذَٰلِكَ دَحَىٰهَآ

Na juu ya hivyo ameitandaza ardhi.


أَخۡرَجَ مِنۡهَا مَآءَهَا وَمَرۡعَىٰهَا

Akatoa ndani yake maji yake na malisho yake,



الصفحة التالية
Icon