فَمَن شَآءَ ذَكَرَهُۥ

Basi anaye penda akumbuke.


فِي صُحُفٖ مُّكَرَّمَةٖ

Yamo katika kurasa zilizo hishimiwa,


مَّرۡفُوعَةٖ مُّطَهَّرَةِۭ

Zilizo inuliwa, zilizo takaswa.


بِأَيۡدِي سَفَرَةٖ

Zimo mikononi mwa Malaika waandishi,


كِرَامِۭ بَرَرَةٖ

Watukufu, wema.


قُتِلَ ٱلۡإِنسَٰنُ مَآ أَكۡفَرَهُۥ

Ameangamia mwanaadamu! Nini kinacho mkufurisha?


مِنۡ أَيِّ شَيۡءٍ خَلَقَهُۥ

Kwa kitu gani amemuumba?


مِن نُّطۡفَةٍ خَلَقَهُۥ فَقَدَّرَهُۥ

Kwa tone la manii, akamuumba na akamkadiria.


ثُمَّ ٱلسَّبِيلَ يَسَّرَهُۥ

Kisha akamsahilishia njia.


ثُمَّ أَمَاتَهُۥ فَأَقۡبَرَهُۥ

Kisha akamfisha, akamtia kaburini.


ثُمَّ إِذَا شَآءَ أَنشَرَهُۥ

Kisha apendapo atamfufua.


كَلَّا لَمَّا يَقۡضِ مَآ أَمَرَهُۥ

La! Hajamaliza aliyo muamuru.



الصفحة التالية
Icon