وَإِذَا ٱلۡجَحِيمُ سُعِّرَتۡ

Na Jahannamu itapo chochewa,


وَإِذَا ٱلۡجَنَّةُ أُزۡلِفَتۡ

Na Pepo ikasogezwa,


عَلِمَتۡ نَفۡسٞ مَّآ أَحۡضَرَتۡ

Kila nafsi itajua ilicho kihudhurisha.


فَلَآ أُقۡسِمُ بِٱلۡخُنَّسِ

Naapa kwa nyota zinapo rejea nyuma,


ٱلۡجَوَارِ ٱلۡكُنَّسِ

Zinazo kwenda, kisha zikajificha,


وَٱلَّيۡلِ إِذَا عَسۡعَسَ

Na kwa usiku unapo pungua,


وَٱلصُّبۡحِ إِذَا تَنَفَّسَ

Na kwa asubuhi inapo pambazuka,


إِنَّهُۥ لَقَوۡلُ رَسُولٖ كَرِيمٖ

Kwamba hakika bila ya shaka hii ni kauli ya Mjumbe mtukufu,


ذِي قُوَّةٍ عِندَ ذِي ٱلۡعَرۡشِ مَكِينٖ

Mwenye nguvu na mwenye cheo kwa huyo Mwenye Kiti cha Enzi,


مُّطَاعٖ ثَمَّ أَمِينٖ

Anaye t'iiwa, tena muaminifu.


وَمَا صَاحِبُكُم بِمَجۡنُونٖ

Na wala huyu mwenzenu hana wazimu.



الصفحة التالية
Icon