ٱلَّذِينَ يُكَذِّبُونَ بِيَوۡمِ ٱلدِّينِ

Ambao wanaikadhibisha Siku ya Malipo.


وَمَا يُكَذِّبُ بِهِۦٓ إِلَّا كُلُّ مُعۡتَدٍ أَثِيمٍ

Wala haikadhibishi ila kila mwenye kuruka mipaka, mwenye dhambi.


إِذَا تُتۡلَىٰ عَلَيۡهِ ءَايَٰتُنَا قَالَ أَسَٰطِيرُ ٱلۡأَوَّلِينَ

Anapo somewa Aya zetu husema: Ni visa vya watu wa kale!


كَلَّاۖ بَلۡۜ رَانَ عَلَىٰ قُلُوبِهِم مَّا كَانُواْ يَكۡسِبُونَ

Hasha! Bali yametia kutu juu ya nyoyo zao hao walio kuwa wakiyachuma.


كَلَّآ إِنَّهُمۡ عَن رَّبِّهِمۡ يَوۡمَئِذٖ لَّمَحۡجُوبُونَ

Hasha! Hakika hao siku hiyo bila ya shaka watazuiliwa na neema za Mola wao Mlezi.


ثُمَّ إِنَّهُمۡ لَصَالُواْ ٱلۡجَحِيمِ

Kisha wataingia Motoni!


ثُمَّ يُقَالُ هَٰذَا ٱلَّذِي كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ

Kisha waambiwe: Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyakadhabisha.


كَلَّآ إِنَّ كِتَٰبَ ٱلۡأَبۡرَارِ لَفِي عِلِّيِّينَ

Hasha! Hakika maandiko ya watu wema bila ya shaka yamo katika I'liyyin.


وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا عِلِّيُّونَ

Na nini kitakacho kujuvya nini I'liyyin?



الصفحة التالية
Icon