كِتَٰبٞ مَّرۡقُومٞ

Kitabu kilicho andikwa.


يَشۡهَدُهُ ٱلۡمُقَرَّبُونَ

Wanakishuhudia walio karibishwa.


إِنَّ ٱلۡأَبۡرَارَ لَفِي نَعِيمٍ

Hakika watu wema bila ya shaka watakuwa katika neema.


عَلَى ٱلۡأَرَآئِكِ يَنظُرُونَ

Wakae juu ya viti vya enzi wakiangalia.


تَعۡرِفُ فِي وُجُوهِهِمۡ نَضۡرَةَ ٱلنَّعِيمِ

Utatambua katika nyuso zao mng'aro wa neema,


يُسۡقَوۡنَ مِن رَّحِيقٖ مَّخۡتُومٍ

Watanyweshwa kinywaji safi kiliyo tiwa muhuri,


خِتَٰمُهُۥ مِسۡكٞۚ وَفِي ذَٰلِكَ فَلۡيَتَنَافَسِ ٱلۡمُتَنَٰفِسُونَ

Muhuri wake ni miski. Na katika hayo washindanie wenye kushindana.


وَمِزَاجُهُۥ مِن تَسۡنِيمٍ

Na mchanganyiko wake ni Tasniim,


عَيۡنٗا يَشۡرَبُ بِهَا ٱلۡمُقَرَّبُونَ

Chemchem watakayo inywa walio kurubishwa.


إِنَّ ٱلَّذِينَ أَجۡرَمُواْ كَانُواْ مِنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ يَضۡحَكُونَ

Kwa hakika wale walio kuwa wakosefu walikuwa wakiwacheka walio amini.



الصفحة التالية
Icon