وَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ وَرَآءَ ظَهۡرِهِۦ

Na ama atakaye pewa daftari lake kwa nyuma ya mgongo wake,


فَسَوۡفَ يَدۡعُواْ ثُبُورٗا

Basi huyo ataomba kuteketea.


وَيَصۡلَىٰ سَعِيرًا

Na ataingia Motoni.


إِنَّهُۥ كَانَ فِيٓ أَهۡلِهِۦ مَسۡرُورًا

Hakika alikuwa furahani kati ya jamaa zake.


إِنَّهُۥ ظَنَّ أَن لَّن يَحُورَ

Huyo hakika alidhani kuwa hatarejea tena.


بَلَىٰٓۚ إِنَّ رَبَّهُۥ كَانَ بِهِۦ بَصِيرٗا

Kwani? Hakika Mola wake Mlezi alikuwa akimwona!


فَلَآ أُقۡسِمُ بِٱلشَّفَقِ

Basi ninaapa kwa wekundu wa jua linapo kuchwa,


وَٱلَّيۡلِ وَمَا وَسَقَ

Na kwa usiku na unavyo vikusanya,


وَٱلۡقَمَرِ إِذَا ٱتَّسَقَ

Na kwa mwezi unapo pevuka,


لَتَرۡكَبُنَّ طَبَقًا عَن طَبَقٖ

Lazima mtapanda t'abaka kwa t'abaka!


فَمَا لَهُمۡ لَا يُؤۡمِنُونَ

Basi wana nini hawaamini?



الصفحة التالية
Icon