وَٱلَّذِي يُمِيتُنِي ثُمَّ يُحۡيِينِ

Na ambaye atanifisha, na kisha atanihuisha.


وَٱلَّذِيٓ أَطۡمَعُ أَن يَغۡفِرَ لِي خَطِيٓـَٔتِي يَوۡمَ ٱلدِّينِ

Na ambaye ndiye ninaye mtumai kunisamehe makosa yangu Siku ya Malipo.


رَبِّ هَبۡ لِي حُكۡمٗا وَأَلۡحِقۡنِي بِٱلصَّـٰلِحِينَ

Mola wangu Mlezi! Nitunukie hukumu na uniunganishe na watendao mema.


وَٱجۡعَل لِّي لِسَانَ صِدۡقٖ فِي ٱلۡأٓخِرِينَ

Na unijaalie nitajwe kwa wema na watu watakao kuja baadaye.


وَٱجۡعَلۡنِي مِن وَرَثَةِ جَنَّةِ ٱلنَّعِيمِ

Na unijaalie katika warithi wa Bustani za neema.


وَٱغۡفِرۡ لِأَبِيٓ إِنَّهُۥ كَانَ مِنَ ٱلضَّآلِّينَ

Na umsamehe baba yangu, kwani hakika alikuwa miongoni mwa wapotovu.


وَلَا تُخۡزِنِي يَوۡمَ يُبۡعَثُونَ

Wala usinihizi Siku watapo fufuliwa.


يَوۡمَ لَا يَنفَعُ مَالٞ وَلَا بَنُونَ

Siku ambayo kwamba mali hayato faa kitu wala wana.


إِلَّا مَنۡ أَتَى ٱللَّهَ بِقَلۡبٖ سَلِيمٖ

Isipo kuwa mwenye kumjia Mwenyezi Mungu na moyo safi.



الصفحة التالية
Icon