وَأُزۡلِفَتِ ٱلۡجَنَّةُ لِلۡمُتَّقِينَ

Na Pepo itasogezwa kwa wachamngu.


وَبُرِّزَتِ ٱلۡجَحِيمُ لِلۡغَاوِينَ

Na Jahannamu itadhihirishwa kwa wapotovu.


وَقِيلَ لَهُمۡ أَيۡنَ مَا كُنتُمۡ تَعۡبُدُونَ

Na wataambiwa: Wako wapi mlio kuwa mkiwaabudu


مِن دُونِ ٱللَّهِ هَلۡ يَنصُرُونَكُمۡ أَوۡ يَنتَصِرُونَ

Badala ya Mwenyezi Mungu? Je! Wanakusaidieni, au wanajisaidia wenyewe?


فَكُبۡكِبُواْ فِيهَا هُمۡ وَٱلۡغَاوُۥنَ

Basi watavurumizwa humo wao na hao wakosefu,


وَجُنُودُ إِبۡلِيسَ أَجۡمَعُونَ

Na majeshi ya Ibilisi yote.


قَالُواْ وَهُمۡ فِيهَا يَخۡتَصِمُونَ

Watasema, na hali ya kuwa wanazozana humo:


تَٱللَّهِ إِن كُنَّا لَفِي ضَلَٰلٖ مُّبِينٍ

Wallahi! Kwa yakini tulikuwa katika upotovu ulio dhaahiri,


إِذۡ نُسَوِّيكُم بِرَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Tulipo kufanyeni ni sawa na Mola Mlezi wa walimwengu wote.


وَمَآ أَضَلَّنَآ إِلَّا ٱلۡمُجۡرِمُونَ

Na hawakutupoteza ila wale wakosefu.



الصفحة التالية
Icon