فَمَا لَنَا مِن شَٰفِعِينَ

Basi hatuna waombezi.


وَلَا صَدِيقٍ حَمِيمٖ

Wala rafiki wa dhati.


فَلَوۡ أَنَّ لَنَا كَرَّةٗ فَنَكُونَ مِنَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Laiti tungeli pata kurejea tena tungeli kuwa katika Waumini.


إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ

Hakika katika haya ipo Ishara, lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.


وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.


كَذَّبَتۡ قَوۡمُ نُوحٍ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Kaumu ya Nuhu waliwakadhibisha Mitume.


إِذۡ قَالَ لَهُمۡ أَخُوهُمۡ نُوحٌ أَلَا تَتَّقُونَ

Alipo waambia ndugu yao, Nuhu: Je! Hamchimngu?


إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ

Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.


فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.


وَمَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ أَجۡرٍۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Na sikutakini juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.



الصفحة التالية
Icon