إِلَّا مَنۡ خَطِفَ ٱلۡخَطۡفَةَ فَأَتۡبَعَهُۥ شِهَابٞ ثَاقِبٞ

Isipo kuwa anaye nyakua kitu kidogo, na mara humfwatia kimondo kinacho ng'ara.


فَٱسۡتَفۡتِهِمۡ أَهُمۡ أَشَدُّ خَلۡقًا أَم مَّنۡ خَلَقۡنَآۚ إِنَّا خَلَقۡنَٰهُم مِّن طِينٖ لَّازِبِۭ

Hebu waulize: Je! Wao ni wenye umbo gumu zaidi au hao wengine tulio waumba. Hakika Sisi tuliwaumba wao kwa udongo unao nata.


بَلۡ عَجِبۡتَ وَيَسۡخَرُونَ

Bali unastaajabu, na wao wanafanya maskhara.


وَإِذَا ذُكِّرُواْ لَا يَذۡكُرُونَ

Na wanapo kumbushwa hawakumbuki.


وَإِذَا رَأَوۡاْ ءَايَةٗ يَسۡتَسۡخِرُونَ

Na wanapo ona Ishara, wanafanya maskhara.


وَقَالُوٓاْ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا سِحۡرٞ مُّبِينٌ

Na husema: Haya si chochote ila ni uchawi tu ulio dhaahiri.


أَءِذَا مِتۡنَا وَكُنَّا تُرَابٗا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَبۡعُوثُونَ

Ati tukisha kufa na tukawa udongo na mifupa ndio kweli tutafufuliwa?


أَوَءَابَآؤُنَا ٱلۡأَوَّلُونَ

Hata baba zetu wa zamani?


قُلۡ نَعَمۡ وَأَنتُمۡ دَٰخِرُونَ

Sema: Naam! Hali nanyi ni madhalili.



الصفحة التالية
Icon