وَيَقُولُونَ أَئِنَّا لَتَارِكُوٓاْ ءَالِهَتِنَا لِشَاعِرٖ مَّجۡنُونِۭ

Na wakisema: Hivyo sisi tuiache miungu yetu kwa ajili ya huyu mtunga mashairi mwendawazimu?


بَلۡ جَآءَ بِٱلۡحَقِّ وَصَدَّقَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Bali huyu amekuja kwa Haki, na amewasadikisha Mitume.


إِنَّكُمۡ لَذَآئِقُواْ ٱلۡعَذَابِ ٱلۡأَلِيمِ

Hakika nyinyi bila ya shaka mtaionja adhabu chungu.


وَمَا تُجۡزَوۡنَ إِلَّا مَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ

Wala hamlipwi ila hayo mliyo kuwa mkiyafanya.


إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلۡمُخۡلَصِينَ

Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.


أُوْلَـٰٓئِكَ لَهُمۡ رِزۡقٞ مَّعۡلُومٞ

Hao ndio watakao pata riziki maalumu,


فَوَٰكِهُ وَهُم مُّكۡرَمُونَ

Matunda, nao watahishimiwa.


فِي جَنَّـٰتِ ٱلنَّعِيمِ

Katika Bustani za neema.


عَلَىٰ سُرُرٖ مُّتَقَٰبِلِينَ

Wako juu ya viti wamekabiliana.


يُطَافُ عَلَيۡهِم بِكَأۡسٖ مِّن مَّعِينِۭ

Wanazungushiwa kikombe chenye kinywaji cha chemchem



الصفحة التالية
Icon