بَيۡضَآءَ لَذَّةٖ لِّلشَّـٰرِبِينَ

Kinywaji cheupe, kitamu kwa wanywao.


لَا فِيهَا غَوۡلٞ وَلَا هُمۡ عَنۡهَا يُنزَفُونَ

Hakina madhara, wala hakiwaleweshi.


وَعِندَهُمۡ قَٰصِرَٰتُ ٱلطَّرۡفِ عِينٞ

Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha mazuri.


كَأَنَّهُنَّ بَيۡضٞ مَّكۡنُونٞ

Hao wanawake kama mayai yaliyo hifadhika.


فَأَقۡبَلَ بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖ يَتَسَآءَلُونَ

Waingie kuulizana wenyewe kwa wenyewe.


قَالَ قَآئِلٞ مِّنۡهُمۡ إِنِّي كَانَ لِي قَرِينٞ

Aseme msemaji mmoja miongoni mwao: Hakika mimi nalikuwa na rafiki


يَقُولُ أَءِنَّكَ لَمِنَ ٱلۡمُصَدِّقِينَ

Aliye kuwa akinambia: Hivyo wewe ni katika wanao sadiki


أَءِذَا مِتۡنَا وَكُنَّا تُرَابٗا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَدِينُونَ

Ati tukisha kufa tukawa udongo na mafupa, ndio tutalipwa na kuhisabiwa?


قَالَ هَلۡ أَنتُم مُّطَّلِعُونَ

Atasema: Je! Nyie mnawaona?



الصفحة التالية
Icon