فَٱطَّلَعَ فَرَءَاهُ فِي سَوَآءِ ٱلۡجَحِيمِ

Basi atachungulia amwone katikati ya Jahannamu.


قَالَ تَٱللَّهِ إِن كِدتَّ لَتُرۡدِينِ

Atasema: Wallahi! Ulikaribia kunipoteza.


وَلَوۡلَا نِعۡمَةُ رَبِّي لَكُنتُ مِنَ ٱلۡمُحۡضَرِينَ

Na lau kuwa si neema ya Mola wangu Mlezi bila ya shaka ningeli kuwa miongoni mwa walio hudhurishwa.


أَفَمَا نَحۡنُ بِمَيِّتِينَ

Je! Sisi hatutakufa,


إِلَّا مَوۡتَتَنَا ٱلۡأُولَىٰ وَمَا نَحۡنُ بِمُعَذَّبِينَ

Isipo kuwa kifo chetu cha kwanza? Wala sisi hatutaadhibiwa.


إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡعَظِيمُ

Hakika huku bila ya shaka ndiko kufuzu kukubwa.


لِمِثۡلِ هَٰذَا فَلۡيَعۡمَلِ ٱلۡعَٰمِلُونَ

Kwa mfano wa haya nawatende watendao.


أَذَٰلِكَ خَيۡرٞ نُّزُلًا أَمۡ شَجَرَةُ ٱلزَّقُّومِ

Je! Kukaribishwa hivi si ndio bora, au mti wa Zaqqum?


إِنَّا جَعَلۡنَٰهَا فِتۡنَةٗ لِّلظَّـٰلِمِينَ

Hakika Sisi tumeufanya huo kuwa ni mateso kwa walio dhulumu.



الصفحة التالية
Icon