ثُمَّ أَغۡرَقۡنَا ٱلۡأٓخَرِينَ

Kisha tukawazamisha wale wengine.


۞وَإِنَّ مِن شِيعَتِهِۦ لَإِبۡرَٰهِيمَ

Na hakika Ibrahim alikuwa katika kundi lake,


إِذۡ جَآءَ رَبَّهُۥ بِقَلۡبٖ سَلِيمٍ

Alipo mjia Mola wake Mlezi kwa moyo mzima.


إِذۡ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوۡمِهِۦ مَاذَا تَعۡبُدُونَ

Alimwambia baba yake na watu wake: Mnaabudu nini?


أَئِفۡكًا ءَالِهَةٗ دُونَ ٱللَّهِ تُرِيدُونَ

Kwa kuzua tu mnataka miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu?


فَمَا ظَنُّكُم بِرَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Mnamdhania nini Mola Mlezi wa walimwengu wote?


فَنَظَرَ نَظۡرَةٗ فِي ٱلنُّجُومِ

Kisha akapiga jicho kutazama nyota.


فَقَالَ إِنِّي سَقِيمٞ

Akasema: Hakika mimi ni mgonjwa!


فَتَوَلَّوۡاْ عَنۡهُ مُدۡبِرِينَ

Nao wakamwacha, wakampa kisogo.


فَرَاغَ إِلَىٰٓ ءَالِهَتِهِمۡ فَقَالَ أَلَا تَأۡكُلُونَ

Basi akaiendea miungu yao kwa siri, akaiambia: Mbona hamli?



الصفحة التالية
Icon