وَتَرَكۡنَا عَلَيۡهِ فِي ٱلۡأٓخِرِينَ

Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu walio kuja baadaye.


سَلَٰمٌ عَلَىٰٓ إِبۡرَٰهِيمَ

Iwe salama kwa Ibrahim!


كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ

Hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.


إِنَّهُۥ مِنۡ عِبَادِنَا ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.


وَبَشَّرۡنَٰهُ بِإِسۡحَٰقَ نَبِيّٗا مِّنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ

Na tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye ni Nabii miongoni mwa watu wema.


وَبَٰرَكۡنَا عَلَيۡهِ وَعَلَىٰٓ إِسۡحَٰقَۚ وَمِن ذُرِّيَّتِهِمَا مُحۡسِنٞ وَظَالِمٞ لِّنَفۡسِهِۦ مُبِينٞ

Na tukambarikia yeye na Is-haqa. Na miongoni mwa dhuriya zao walitokea wema na wenye kudhulumu nafsi zao waziwazi.


وَلَقَدۡ مَنَنَّا عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَٰرُونَ

Na kwa hakika tuliwafanyia hisani Musa na Haruni.


وَنَجَّيۡنَٰهُمَا وَقَوۡمَهُمَا مِنَ ٱلۡكَرۡبِ ٱلۡعَظِيمِ

Na tukawaokoa wao na watu wao kutokana na dhiki kubwa.


وَنَصَرۡنَٰهُمۡ فَكَانُواْ هُمُ ٱلۡغَٰلِبِينَ

Na tukawanusuru; na wakawa wao ndio wenye kushinda.



الصفحة التالية
Icon