وَءَاتَيۡنَٰهُمَا ٱلۡكِتَٰبَ ٱلۡمُسۡتَبِينَ

Na tukawapa wawili hao Kitabu kinacho bainisha.


وَهَدَيۡنَٰهُمَا ٱلصِّرَٰطَ ٱلۡمُسۡتَقِيمَ

Na tukawaongoa kwenye Njia Iliyo Nyooka.


وَتَرَكۡنَا عَلَيۡهِمَا فِي ٱلۡأٓخِرِينَ

Na tukawaachia (sifa njema) katika watu walio kuja baadaye.


سَلَٰمٌ عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَٰرُونَ

Iwe salama kwa Musa na Haruni!


إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ

Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema.


إِنَّهُمَا مِنۡ عِبَادِنَا ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Hakika wawili hao ni katika waja wetu walio amini.


وَإِنَّ إِلۡيَاسَ لَمِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Na hakika Ilyas bila ya shaka alikuwa miongoni mwa Mitume.


إِذۡ قَالَ لِقَوۡمِهِۦٓ أَلَا تَتَّقُونَ

Alipo waambia watu wake: Hamwogopi?


أَتَدۡعُونَ بَعۡلٗا وَتَذَرُونَ أَحۡسَنَ ٱلۡخَٰلِقِينَ

Mnamwomba Baa'li na mnamwacha Mbora wa waumbaji,


ٱللَّهَ رَبَّكُمۡ وَرَبَّ ءَابَآئِكُمُ ٱلۡأَوَّلِينَ

Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa zamani?



الصفحة التالية
Icon