وَأَنۢبَتۡنَا عَلَيۡهِ شَجَرَةٗ مِّن يَقۡطِينٖ

Na tukauotesha juu yake mmea wa kabila ya mung'unye.


وَأَرۡسَلۡنَٰهُ إِلَىٰ مِاْئَةِ أَلۡفٍ أَوۡ يَزِيدُونَ

Na tulimtuma kwa watu laki moja au zaidi.


فَـَٔامَنُواْ فَمَتَّعۡنَٰهُمۡ إِلَىٰ حِينٖ

Basi wakaamini, na tukawastarehesha kwa muda.


فَٱسۡتَفۡتِهِمۡ أَلِرَبِّكَ ٱلۡبَنَاتُ وَلَهُمُ ٱلۡبَنُونَ

Basi waulize: Ati Mola wako Mlezi ndiye mwenye watoto wa kike, na wao wanao watoto wa kiume?


أَمۡ خَلَقۡنَا ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةَ إِنَٰثٗا وَهُمۡ شَٰهِدُونَ

Au tumewaumba Malaika kuwa ni wanawake, na wao wakashuhudia?


أَلَآ إِنَّهُم مِّنۡ إِفۡكِهِمۡ لَيَقُولُونَ

Ati ni kwa uzushi wao ndio wanasema:


وَلَدَ ٱللَّهُ وَإِنَّهُمۡ لَكَٰذِبُونَ

Mwenyezi Mungu amezaa! Ama hakika bila ya shaka hao ni waongo!


أَصۡطَفَى ٱلۡبَنَاتِ عَلَى ٱلۡبَنِينَ

Ati amekhiari watoto wa kike kuliko wanaume?


مَا لَكُمۡ كَيۡفَ تَحۡكُمُونَ

Mna nini? Mnahukumu vipi nyinyi?



الصفحة التالية
Icon