أَفَلَا تَذَكَّرُونَ

Hamkumbuki?


أَمۡ لَكُمۡ سُلۡطَٰنٞ مُّبِينٞ

Au mnayo hoja iliyo wazi?


فَأۡتُواْ بِكِتَٰبِكُمۡ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ

Basi leteni Kitabu chenu kama mnasema kweli.


وَجَعَلُواْ بَيۡنَهُۥ وَبَيۡنَ ٱلۡجِنَّةِ نَسَبٗاۚ وَلَقَدۡ عَلِمَتِ ٱلۡجِنَّةُ إِنَّهُمۡ لَمُحۡضَرُونَ

Na wameweka makhusiano ya nasaba baina yake na majini; na majini wamekwisha jua bila ya shaka kuwa wao watahudhurishwa.


سُبۡحَٰنَ ٱللَّهِ عَمَّا يَصِفُونَ

Subhana 'Llah Ametakasika Mwenyezi Mungu na hayo wanayo msingizia.


إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلۡمُخۡلَصِينَ

Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa.


فَإِنَّكُمۡ وَمَا تَعۡبُدُونَ

Basi hakika nyinyi na mnao waabudu


مَآ أَنتُمۡ عَلَيۡهِ بِفَٰتِنِينَ

Hamwezi kuwapoteza


إِلَّا مَنۡ هُوَ صَالِ ٱلۡجَحِيمِ

Isipo kuwa yule atakaye ingia Motoni.


وَمَامِنَّآ إِلَّا لَهُۥ مَقَامٞ مَّعۡلُومٞ

Na hapana katika sisi ila anapo mahali pake maalumu.



الصفحة التالية
Icon