وَأَنَّهُۥ هُوَ أَضۡحَكَ وَأَبۡكَىٰ

Na kwamba Yeye ndiye anaye leta kicheko na kilio.


وَأَنَّهُۥ هُوَ أَمَاتَ وَأَحۡيَا

Na kwamba Yeye ndiye anaye fisha na kuhuisha.


وَأَنَّهُۥ خَلَقَ ٱلزَّوۡجَيۡنِ ٱلذَّكَرَ وَٱلۡأُنثَىٰ

Na kwamba Yeye ndiye aliye umba jozi, dume na jike


مِن نُّطۡفَةٍ إِذَا تُمۡنَىٰ

Kutokana na mbegu ya uzazi inapo miminwa.


وَأَنَّ عَلَيۡهِ ٱلنَّشۡأَةَ ٱلۡأُخۡرَىٰ

Na kwamba ni juu yake ufufuo mwengine.


وَأَنَّهُۥ هُوَ أَغۡنَىٰ وَأَقۡنَىٰ

Na kwamba ni Yeye ndiye anaye tosheleza na kukinaisha.


وَأَنَّهُۥ هُوَ رَبُّ ٱلشِّعۡرَىٰ

Na kwamba hakika Yeye ndiye Mola Mlezi wa nyota ya Shii'ra.


وَأَنَّهُۥٓ أَهۡلَكَ عَادًا ٱلۡأُولَىٰ

Na kwamba Yeye ndiye aliye waangamiza A'di wa kwanza,


وَثَمُودَاْ فَمَآ أَبۡقَىٰ

Na Thamudi hakuwabakisha,


وَقَوۡمَ نُوحٖ مِّن قَبۡلُۖ إِنَّهُمۡ كَانُواْ هُمۡ أَظۡلَمَ وَأَطۡغَىٰ

Na kabla yao kaumu ya Nuhu. Na hao hakika walikuwa ni madhaalimu zaidi, na waovu zaidi;



الصفحة التالية
Icon