وَٱلۡحَبُّ ذُو ٱلۡعَصۡفِ وَٱلرَّيۡحَانُ

Na nafaka zenye makapi, na rehani.


فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha


خَلَقَ ٱلۡإِنسَٰنَ مِن صَلۡصَٰلٖ كَٱلۡفَخَّارِ

Amemuumba mtu kwa udongo wa kinamo..


وَخَلَقَ ٱلۡجَآنَّ مِن مَّارِجٖ مِّن نَّارٖ

Na akawaumba majini kwa ulimi wa moto.


فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha


رَبُّ ٱلۡمَشۡرِقَيۡنِ وَرَبُّ ٱلۡمَغۡرِبَيۡنِ

Mola Mlezi wa mashariki mbili na wa magharibi mbili.


فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?


مَرَجَ ٱلۡبَحۡرَيۡنِ يَلۡتَقِيَانِ

Anaziendesha bahari mbili zikutane;


بَيۡنَهُمَا بَرۡزَخٞ لَّا يَبۡغِيَانِ

Baina yao kipo kizuizi, zisiingiliane.


فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?



الصفحة التالية
Icon