As-Saffat


وَٱلصَّـٰٓفَّـٰتِ صَفّٗا

Naapa kwa wanao jipanga kwa safu.


فَٱلزَّـٰجِرَٰتِ زَجۡرٗا

Na kwa wenye kukataza mabaya.


فَٱلتَّـٰلِيَٰتِ ذِكۡرًا

Na kwa wenye kusoma Ukumbusho.


إِنَّ إِلَٰهَكُمۡ لَوَٰحِدٞ

Hakika Mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja.


رَّبُّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَا وَرَبُّ ٱلۡمَشَٰرِقِ

Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na yaliyomo kati yao, na ni Mola Mlezi wa mashariki zote.


إِنَّا زَيَّنَّا ٱلسَّمَآءَ ٱلدُّنۡيَا بِزِينَةٍ ٱلۡكَوَاكِبِ

Hakika Sisi tumeipamba mbingu ya karibu kwa pambo la nyota.


وَحِفۡظٗا مِّن كُلِّ شَيۡطَٰنٖ مَّارِدٖ

Na kulinda na kila shet'ani a'si.


لَّا يَسَّمَّعُونَ إِلَى ٱلۡمَلَإِ ٱلۡأَعۡلَىٰ وَيُقۡذَفُونَ مِن كُلِّ جَانِبٖ

Wasiweze kuwasikiliza viumbe watukufu. Na wanafukuzwa huko kila upande.


دُحُورٗاۖ وَلَهُمۡ عَذَابٞ وَاصِبٌ

Wakifurushwa. Na wanayo adhabu ya kudumu.



الصفحة التالية
Icon