Az-Zariyat


وَٱلذَّـٰرِيَٰتِ ذَرۡوٗا

Naapa kwa pepo zinazo tawanya,


فَٱلۡحَٰمِلَٰتِ وِقۡرٗا

Na zinazo beba mizigo,


فَٱلۡجَٰرِيَٰتِ يُسۡرٗا

Na zinazo kwenda kwa wepesi.


فَٱلۡمُقَسِّمَٰتِ أَمۡرًا

Na zinazo gawanya kwa amri,


إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَصَادِقٞ

Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka ni kweli,


وَإِنَّ ٱلدِّينَ لَوَٰقِعٞ

Na kwa hakika malipo bila ya shaka yatatokea.


وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلۡحُبُكِ

Naapa kwa mbingu zenye njia,


إِنَّكُمۡ لَفِي قَوۡلٖ مُّخۡتَلِفٖ

Hakika nyinyi bila ya shaka mmo katika kauli inayo khitalifiana.


يُؤۡفَكُ عَنۡهُ مَنۡ أُفِكَ

Anageuzwa kutokana na haki mwenye kugeuzwa.


قُتِلَ ٱلۡخَرَّـٰصُونَ

Wazushi wameangamizwa.


ٱلَّذِينَ هُمۡ فِي غَمۡرَةٖ سَاهُونَ

Ambao wameghafilika katika ujinga.



الصفحة التالية
Icon