An-Najm


وَٱلنَّجۡمِ إِذَا هَوَىٰ

Naapa kwa nyota inapo tua,


مَا ضَلَّ صَاحِبُكُمۡ وَمَا غَوَىٰ

Mwenzenu huyu hakupotea, wala hakukosea.


وَمَا يَنطِقُ عَنِ ٱلۡهَوَىٰٓ

Wala hatamki kwa matamanio.


إِنۡ هُوَ إِلَّا وَحۡيٞ يُوحَىٰ

Hayakuwa haya ila ni ufunuo ulio funuliwa;


عَلَّمَهُۥ شَدِيدُ ٱلۡقُوَىٰ

Amemfundisha aliye mwingi wa nguvu,


ذُو مِرَّةٖ فَٱسۡتَوَىٰ

Mwenye kutua, akatulia,


وَهُوَ بِٱلۡأُفُقِ ٱلۡأَعۡلَىٰ

Naye yuko juu kabisa upeo wa macho.


ثُمَّ دَنَا فَتَدَلَّىٰ

Kisha akakaribia na akateremka.


فَكَانَ قَابَ قَوۡسَيۡنِ أَوۡ أَدۡنَىٰ

Akawa ni kama baina ya mipinde miwili, au karibu zaidi.


فَأَوۡحَىٰٓ إِلَىٰ عَبۡدِهِۦ مَآ أَوۡحَىٰ

Akamfunulia mja wake (Mwenyezi Mungu) alicho mfunulia.


مَا كَذَبَ ٱلۡفُؤَادُ مَا رَأَىٰٓ

Moyo haukusema uwongo uliyo yaona.



الصفحة التالية
Icon