Ar-Rahman


ٱلرَّحۡمَٰنُ

Arrah'man, Mwingi wa Rehema


عَلَّمَ ٱلۡقُرۡءَانَ

Amefundisha Qur'ani.


خَلَقَ ٱلۡإِنسَٰنَ

Amemuumba mwanaadamu,


عَلَّمَهُ ٱلۡبَيَانَ

Akamfundisha kubaini.


ٱلشَّمۡسُ وَٱلۡقَمَرُ بِحُسۡبَانٖ

Jua na mwezi huenda kwa hisabu.


وَٱلنَّجۡمُ وَٱلشَّجَرُ يَسۡجُدَانِ

Na mimea yenye kutambaa, na miti, inanyenyekea.


وَٱلسَّمَآءَ رَفَعَهَا وَوَضَعَ ٱلۡمِيزَانَ

Na mbingu ameziinua, na ameweka mizani,


أَلَّا تَطۡغَوۡاْ فِي ٱلۡمِيزَانِ

Ili msidhulumu katika mizani.


وَأَقِيمُواْ ٱلۡوَزۡنَ بِٱلۡقِسۡطِ وَلَا تُخۡسِرُواْ ٱلۡمِيزَانَ

Na wekeni mizani kwa haki, wala msipunje katika mizani.


وَٱلۡأَرۡضَ وَضَعَهَا لِلۡأَنَامِ

Na ardhi ameiweka kwa ajili ya viumbe.


فِيهَا فَٰكِهَةٞ وَٱلنَّخۡلُ ذَاتُ ٱلۡأَكۡمَامِ

Humo yamo matunda na mitende yenye mafumba.



الصفحة التالية
Icon