Al-Kalam


نٓۚ وَٱلۡقَلَمِ وَمَا يَسۡطُرُونَ

Nuun. Naapa kwa kalamu na yale wayaandikayo,


مَآ أَنتَ بِنِعۡمَةِ رَبِّكَ بِمَجۡنُونٖ

Kwa neema ya Mola wako Mlezi wewe si mwendawazimu.


وَإِنَّ لَكَ لَأَجۡرًا غَيۡرَ مَمۡنُونٖ

Na kwa hakika wewe una malipo yasiyo katika.


وَإِنَّكَ لَعَلَىٰ خُلُقٍ عَظِيمٖ

Na hakika wewe una tabia tukufu.


فَسَتُبۡصِرُ وَيُبۡصِرُونَ

Karibu utaona, na wao wataona,


بِأَييِّكُمُ ٱلۡمَفۡتُونُ

Ni nani kati yenu aliye pandwa na wazimu.


إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعۡلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِۦ وَهُوَ أَعۡلَمُ بِٱلۡمُهۡتَدِينَ

Hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye ajuaye zaidi nani aliye ipotea Njia yake, na Yeye ndiye anaye wajua zaidi walio ongoka.


فَلَا تُطِعِ ٱلۡمُكَذِّبِينَ

Basi usiwat'ii wanao kadhibisha.


وَدُّواْ لَوۡ تُدۡهِنُ فَيُدۡهِنُونَ

Wanatamani lau unge lainisha ili nao wakulainishie.



الصفحة التالية
Icon