Al-Ma'arij


سَأَلَ سَآئِلُۢ بِعَذَابٖ وَاقِعٖ

Muulizaji aliuliza juu ya adhabu itakayo tokea,


لِّلۡكَٰفِرِينَ لَيۡسَ لَهُۥ دَافِعٞ

Kwa makafiri - ambayo hapana awezaye kuizuia -


مِّنَ ٱللَّهِ ذِي ٱلۡمَعَارِجِ

Kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mwenye mbingu za daraja.


تَعۡرُجُ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ وَٱلرُّوحُ إِلَيۡهِ فِي يَوۡمٖ كَانَ مِقۡدَارُهُۥ خَمۡسِينَ أَلۡفَ سَنَةٖ

Malaika na Roho hupanda kwendea kwake katika siku ambayo kadiri yake ni miaka khamsini elfu!


فَٱصۡبِرۡ صَبۡرٗا جَمِيلًا

Basi subiri kwa subira njema.


إِنَّهُمۡ يَرَوۡنَهُۥ بَعِيدٗا

Hakika wao wanaiona iko mbali,


وَنَرَىٰهُ قَرِيبٗا

Na Sisi tunaiona iko karibu.


يَوۡمَ تَكُونُ ٱلسَّمَآءُ كَٱلۡمُهۡلِ

Siku ambayo mbingu zitakapo kuwa kama maadeni iliyo yayushwa.


وَتَكُونُ ٱلۡجِبَالُ كَٱلۡعِهۡنِ

Na milima itakuwa kama sufi.


وَلَا يَسۡـَٔلُ حَمِيمٌ حَمِيمٗا

Wala jamaa hatamuuliza jamaa yake.



الصفحة التالية
Icon