Al-Muddasir


يَـٰٓأَيُّهَا ٱلۡمُدَّثِّرُ

Ewe uliye jigubika!


قُمۡ فَأَنذِرۡ

Simama uonye!


وَرَبَّكَ فَكَبِّرۡ

Na Mola wako Mlezi mtukuze!


وَثِيَابَكَ فَطَهِّرۡ

Na nguo zako, zisafishe.


وَٱلرُّجۡزَ فَٱهۡجُرۡ

Na yaliyo machafu yahame!


وَلَا تَمۡنُن تَسۡتَكۡثِرُ

Wala usitoe kwa kutaraji kuzidishiwa.


وَلِرَبِّكَ فَٱصۡبِرۡ

Na kwa ajili ya Mola wako Mlezi, subiri!


فَإِذَا نُقِرَ فِي ٱلنَّاقُورِ

Basi litapo pulizwa barugumu,


فَذَٰلِكَ يَوۡمَئِذٖ يَوۡمٌ عَسِيرٌ

Siku hiyo, basi, itakuwa siku ngumu.


عَلَى ٱلۡكَٰفِرِينَ غَيۡرُ يَسِيرٖ

Kwa makafiri haitakuwa nyepesi.


ذَرۡنِي وَمَنۡ خَلَقۡتُ وَحِيدٗا

Niache peke yangu na niliye muumba;


وَجَعَلۡتُ لَهُۥ مَالٗا مَّمۡدُودٗا

Na nikamjaalia awe na mali mengi,



الصفحة التالية
Icon