Al-Kiyama


لَآ أُقۡسِمُ بِيَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ

Ninaapa kwa Siku ya Kiyama!


وَلَآ أُقۡسِمُ بِٱلنَّفۡسِ ٱللَّوَّامَةِ

Na ninaapa kwa nafsi inayo jilaumu!


أَيَحۡسَبُ ٱلۡإِنسَٰنُ أَلَّن نَّجۡمَعَ عِظَامَهُۥ

Anadhani mtu kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake?


بَلَىٰ قَٰدِرِينَ عَلَىٰٓ أَن نُّسَوِّيَ بَنَانَهُۥ

Kwani! Sisi tunaweza hata kuziweka sawa sawa ncha za vidole vyake!


بَلۡ يُرِيدُ ٱلۡإِنسَٰنُ لِيَفۡجُرَ أَمَامَهُۥ

Lakini mtu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilioko mbele yake.


يَسۡـَٔلُ أَيَّانَ يَوۡمُ ٱلۡقِيَٰمَةِ

Anauliza: Lini itakuwa hiyo Siku ya Kiyama?


فَإِذَا بَرِقَ ٱلۡبَصَرُ

Basi jicho litapo dawaa,


وَخَسَفَ ٱلۡقَمَرُ

Na mwezi utapo patwa,


وَجُمِعَ ٱلشَّمۡسُ وَٱلۡقَمَرُ

Na likakusanywa jua na mwezi,


يَقُولُ ٱلۡإِنسَٰنُ يَوۡمَئِذٍ أَيۡنَ ٱلۡمَفَرُّ

Siku hiyo mtu atasema: Yako wapi makimbilio?



الصفحة التالية
Icon