An-Naba'i


عَمَّ يَتَسَآءَلُونَ

WANAULIZANA nini?


عَنِ ٱلنَّبَإِ ٱلۡعَظِيمِ

Ile khabari kuu,


ٱلَّذِي هُمۡ فِيهِ مُخۡتَلِفُونَ

Ambayo kwayo wanakhitalifiana.


كَلَّا سَيَعۡلَمُونَ

La! Karibu watakuja jua.


ثُمَّ كَلَّا سَيَعۡلَمُونَ

Tena la! Karibu watakuja jua.


أَلَمۡ نَجۡعَلِ ٱلۡأَرۡضَ مِهَٰدٗا

Kwani hatukuifanya ardhi kama tandiko?


وَٱلۡجِبَالَ أَوۡتَادٗا

Na milima kama vigingi?


وَخَلَقۡنَٰكُمۡ أَزۡوَٰجٗا

Na tukakuumbeni kwa jozi?


وَجَعَلۡنَا نَوۡمَكُمۡ سُبَاتٗا

Na tukakufanya kulala kwenu ni mapumziko?


وَجَعَلۡنَا ٱلَّيۡلَ لِبَاسٗا

Na tukaufanya usiku ni nguo?


وَجَعَلۡنَا ٱلنَّهَارَ مَعَاشٗا

Na tukaufanya mchana ni wa kuchumia maisha?



الصفحة التالية
Icon