An-Nazi'at


وَٱلنَّـٰزِعَٰتِ غَرۡقٗا

Naapa kwa wanao komoa kwa nguvu,


وَٱلنَّـٰشِطَٰتِ نَشۡطٗا

Na kwa wanao toa kwa upole,


وَٱلسَّـٰبِحَٰتِ سَبۡحٗا

Na wanao ogelea,


فَٱلسَّـٰبِقَٰتِ سَبۡقٗا

Wakishindana mbio,


فَٱلۡمُدَبِّرَٰتِ أَمۡرٗا

Wakidabiri mambo.


يَوۡمَ تَرۡجُفُ ٱلرَّاجِفَةُ

Siku kitapo tetemeka cha kutetemeka,


تَتۡبَعُهَا ٱلرَّادِفَةُ

Kifuate cha kufuatia.


قُلُوبٞ يَوۡمَئِذٖ وَاجِفَةٌ

Siku hiyo nyoyo zitapiga piga,


أَبۡصَٰرُهَا خَٰشِعَةٞ

Macho yatainama chini.


يَقُولُونَ أَءِنَّا لَمَرۡدُودُونَ فِي ٱلۡحَافِرَةِ

Sasa wanasema: Ati kweli tutarudishwa kwenye hali ya kwanza?


أَءِذَا كُنَّا عِظَٰمٗا نَّخِرَةٗ

Hata tukiwa mifupa iliyo bunguliwa?



الصفحة التالية
Icon