Al-Mutaffifin


وَيۡلٞ لِّلۡمُطَفِّفِينَ

Ole wao hao wapunjao!


ٱلَّذِينَ إِذَا ٱكۡتَالُواْ عَلَى ٱلنَّاسِ يَسۡتَوۡفُونَ

Ambao wanapo jipimia kwa watu hudai watimiziwe.


وَإِذَا كَالُوهُمۡ أَو وَّزَنُوهُمۡ يُخۡسِرُونَ

Na wao wanapo wapimia watu kwa kipimo au mizani hupunguza.


أَلَا يَظُنُّ أُوْلَـٰٓئِكَ أَنَّهُم مَّبۡعُوثُونَ

Kwani hawadhani hao kwamba watafufuliwa


لِيَوۡمٍ عَظِيمٖ

Katika Siku iliyo kuu,


يَوۡمَ يَقُومُ ٱلنَّاسُ لِرَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Siku watapo msimamia watu Mola Mlezi wa walimwengu wote?


كَلَّآ إِنَّ كِتَٰبَ ٱلۡفُجَّارِ لَفِي سِجِّينٖ

Hasha! Hakika maandiko ya wakosefu bila ya shaka yamo katika Sijjin.


وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا سِجِّينٞ

Unajua nini Sijjin?


كِتَٰبٞ مَّرۡقُومٞ

Kitabu kilicho andikwa.


وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo kwa wanao kadhibisha!



الصفحة التالية
Icon