Al-Inshikak


إِذَا ٱلسَّمَآءُ ٱنشَقَّتۡ

Itapo chanika mbingu,


وَأَذِنَتۡ لِرَبِّهَا وَحُقَّتۡ

Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,


وَإِذَا ٱلۡأَرۡضُ مُدَّتۡ

Na ardhi itakapo tanuliwa,


وَأَلۡقَتۡ مَا فِيهَا وَتَخَلَّتۡ

Na kuvitoa vilivyo kuwa ndani yake, ikawa tupu,


وَأَذِنَتۡ لِرَبِّهَا وَحُقَّتۡ

Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,


يَـٰٓأَيُّهَا ٱلۡإِنسَٰنُ إِنَّكَ كَادِحٌ إِلَىٰ رَبِّكَ كَدۡحٗا فَمُلَٰقِيهِ

Ewe mtu! Hakika wewe unajikusuru kwa juhudi kumwendea Mola wako Mlezi, basi utamkuta.


فَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ بِيَمِينِهِۦ

Ama atakaye pewa daftari lake kwa mkono wa kulia,


فَسَوۡفَ يُحَاسَبُ حِسَابٗا يَسِيرٗا

Basi huyo atahisabiwa hisabu nyepesi,


وَيَنقَلِبُ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِۦ مَسۡرُورٗا

Na arudi kwa ahali zake na furaha.



الصفحة التالية
Icon