Al'A'alah


سَبِّحِ ٱسۡمَ رَبِّكَ ٱلۡأَعۡلَى

Litakase jina la Mola wako Mlezi aliye juu kabisa,


ٱلَّذِي خَلَقَ فَسَوَّىٰ

Aliye umba, na akaweka sawa,


وَٱلَّذِي قَدَّرَ فَهَدَىٰ

Na ambaye amekadiria na akaongoa,


وَٱلَّذِيٓ أَخۡرَجَ ٱلۡمَرۡعَىٰ

Na aliye otesha malisho,


فَجَعَلَهُۥ غُثَآءً أَحۡوَىٰ

Kisha akayafanya makavu, meusi.


سَنُقۡرِئُكَ فَلَا تَنسَىٰٓ

Tutakusomesha wala hutasahau,


إِلَّا مَا شَآءَ ٱللَّهُۚ إِنَّهُۥ يَعۡلَمُ ٱلۡجَهۡرَ وَمَا يَخۡفَىٰ

Ila akipenda Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye anayajua yaliyo dhaahiri na yaliyo fichikana.


وَنُيَسِّرُكَ لِلۡيُسۡرَىٰ

Na tutakusahilishia yawe mepesi.


فَذَكِّرۡ إِن نَّفَعَتِ ٱلذِّكۡرَىٰ

Basi kumbusha, kama kukumbusha kunafaa.


سَيَذَّكَّرُ مَن يَخۡشَىٰ

Atakumbuka mwenye kuogopa.



الصفحة التالية
Icon