Al-Balad


لَآ أُقۡسِمُ بِهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ

Naapa kwa Mji huu!


وَأَنتَ حِلُّۢ بِهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ

Nawe unaukaa Mji huu.


وَوَالِدٖ وَمَا وَلَدَ

Na naapa kwa mzazi na alicho kizaa.


لَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ فِي كَبَدٍ

Hakika tumemuumba mtu katika taabu.


أَيَحۡسَبُ أَن لَّن يَقۡدِرَ عَلَيۡهِ أَحَدٞ

Ati anadhani hapana yeyote ataye muweza?


يَقُولُ أَهۡلَكۡتُ مَالٗا لُّبَدًا

Anasema: Nimeteketeza chungu ya mali.


أَيَحۡسَبُ أَن لَّمۡ يَرَهُۥٓ أَحَدٌ

Ati anadhani ya kuwa hapana yeyote anaye mwona?


أَلَمۡ نَجۡعَل لَّهُۥ عَيۡنَيۡنِ

Kwani hatukumpa macho mawili?


وَلِسَانٗا وَشَفَتَيۡنِ

Na ulimi, na midomo miwili?


وَهَدَيۡنَٰهُ ٱلنَّجۡدَيۡنِ

Na tukambainishia zote njia mbili?


فَلَا ٱقۡتَحَمَ ٱلۡعَقَبَةَ

Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani.



الصفحة التالية
Icon