Al-Lail


وَٱلَّيۡلِ إِذَا يَغۡشَىٰ

Naapa kwa usiku unapo funika!


وَٱلنَّهَارِ إِذَا تَجَلَّىٰ

Na mchana unapo dhihiri!


وَمَا خَلَقَ ٱلذَّكَرَ وَٱلۡأُنثَىٰٓ

Na kwa Aliye umba dume na jike!


إِنَّ سَعۡيَكُمۡ لَشَتَّىٰ

Hakika juhudi zenu bila ya shaka ni mbali mbali.


فَأَمَّا مَنۡ أَعۡطَىٰ وَٱتَّقَىٰ

Ama mwenye kutoa na akamchamngu,


وَصَدَّقَ بِٱلۡحُسۡنَىٰ

Na akaliwafiki lilio jema,


فَسَنُيَسِّرُهُۥ لِلۡيُسۡرَىٰ

Tutamsahilishia yawe mepesi.


وَأَمَّا مَنۢ بَخِلَ وَٱسۡتَغۡنَىٰ

Na ama mwenye kufanya ubakhili, na asiwe na haja ya wenzake,


وَكَذَّبَ بِٱلۡحُسۡنَىٰ

Na akakanusha lilio jema,


فَسَنُيَسِّرُهُۥ لِلۡعُسۡرَىٰ

Tutamsahilishia yawe mazito!


وَمَا يُغۡنِي عَنۡهُ مَالُهُۥٓ إِذَا تَرَدَّىٰٓ

Na mali yake yatamfaa nini atapo kuwa anadidimia?



الصفحة التالية
Icon